Kazi na Mamlaka ya Tume
Kazi za Tume
Kwa mujibu wa vifungu namba 12, 13 na 37 vya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma , kazi na majukumu ya Tume ni pamoja na:
-
-
- Kupokea na kuhifadhi Tamko la Taarifa za Mali na Madeni linalowasilishwa na Kiongozi wa Umma kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
- Kupokea tuhuma na taarifa za uvunjwaji wa maadili kutoka kwa wananchi;
- Kufanya uchunguzi juu ya madai au tuhuma za uvunjwaji wa maadili dhidi ya Kiongozi yeyote wa Umma;
- Kupokea, kuchunguza na kushughulikia madai yote yanayohusu uvunjwaji wa maadili katika taasisi za umma;
- Kuchunguza mwenendo wa Kiongozi yeyote wa Umma ambao kwa maoni ya Tume, unapelekea au unachangia uvunjwaji wa maadili chini ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
- Kusikiliza na kutoa maamuzi kuhusu madai yoyote ya uvunjwaji wa maadili dhidi ya Kiongozi wa Umma; na
- Kuelimisha umma juu ya umuhimu wa maadili.
-
Uwezo wa Tume
-
-
- Kumuagiza ofisa yeyote wa Tume kufanya uchunguzi wa tuhuma yoyote ya uvunjwaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Sheria Nam. 4 ya mwaka 2015;
- Kumtaka kwa maandishi, mtu yeyote au taasisi yoyote kutoa au kuwasilisha taarifa au kujibu maswali au kuwasilisha kumbukumbu au nyaraka zozote zinazohusiana na tuhuma zinazohitaji kufanyiwa uchunguzi; na
- Kuchunguza Akaunti yoyote ya Benki ambayo Tume inataka kujiridhisha kuhusu hesabu zake, hesabu za hisa, hesabu za manunuzi au nyaraka zozote zinazohusiana na akiba au amana.
-